Monday 12 February 2018

ANC kutoa maamuzi magumu leo

Viongozi wakuu wa chama tawala nchini Afrika Kusini - cha African National Congress, ANC wanakutana hii leo kwa kile kinachotajwa kuwa ni "kumalizia" hatua za kumuondoa rais wa taifa hilo Jacob Zuma.
Viongozi wakuu wa chama tawala nchini Afrika Kusini - cha African National Congress, ANC wanakutana hii leo kwa kile kinachotajwa kuwa ni "kumalizia" hatua za kumuondoa rais wa taifa hilo Jacob Zuma baada ya kiongozi wake Cyril Ramaphosa kuahidi kuutamatisha mzozo huo.
Ramaphosa alisema katika mkutano wa chama cha ANC mjini Cape town jana Jumapili kwamba alitaka kubadilisha kile alichokiita "kipindi kigumu, mgawanyiko na kutoelewana, na kuleta mwanzo mpya kwa chama hicho".
Ramaphosa alisema, huku akishangiliwa kwa makofi kwamba anafahamu umma unataka suala hilo kufikia tamati, akiapa kupambana na rushwa iliyoharibu sifa ya serikali ya rais Jacob Zuma.
Zuma ameendelea kung'ang'ania madarakani baada ya kukataa ombi kutoka maafisa waandamaizi wa chama chake la kumtaka ajiuzulu mnamo wiki iliyopita.
Kamati kuu ambayo ina nguvu zaidi kwenye chama hicho inaweza kumtaka kuachia wadhifa wake, ingawa hawajibiki kwa namna yoyote kikatiba kuheshimu agizo la kamati hiyo.

0 comments:

Post a Comment