Friday 23 February 2018

Kenya na Tanzania kumaliza migogoro iliyokuwepo



 Rais John Pombe Magufuli na Rais Uhuru Kenyatta wamewaagiza Mawaziri wao kumaliza tofauti ndogondogo za kibiashara baina ya Tanzania na Kenya
-
Marais hao wamesema wanataka kuona biashara inazidi kukua na bidhaa zinanunuliwa na kuuzwa bila vikwazo vyovyote baina ya nchi hizo
-
Wametoa maagizo hayo kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania Dkt. Agustine Mahiga na Waziri wa Katiba na Sheria wa Tanzania Prof. Palamagamba Kabudi
-
Pia maagizo hayo yametolewa kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Monica Juma na Waziri wa Afrika Mashariki na Maendeleo ya Ushoroba wa Kaskazini wa Kenya Peter Munya

0 comments:

Post a Comment