Monday 26 February 2018

Man City waipiga Arsenal 3-0 na kutwaa kombe la Ligi England


Klabu ya Manchester City chini ya kocha wake Pep Guardiola usiku wa jana imefanikiwa kutwaa taji lake la kwanza msimu wa 2017/2018 dhidi ya Arsenal katika fainali ya kombe la Carabao uliopigwa uwanja wa Wembley jijini London. Man City imeshinda goli 3-0, magoli ambayo yamefungwa na Sergio Aguero dakika ya 18, Vincent Kompany dakika ya 58 huku David Silva akishindilia msumari wa moto kwa kufunga goli la tatu dakika ya 65.

0 comments:

Post a Comment