Monday 26 February 2018

Mhambulizi Syria yanatisha

Serikali ya Syria imefanya mashambulizi makubwa ya anga na ardhini katika maeneo yanayodhibitiwa na waasi Ghouta Mashariki, siku moja baada ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kutaka kusitishwa haraka mapigano.
Shirika linalofuatilia haki za binaadamu nchini Syria lenye makao yake Uingereza, limesema kuwa kiasi ya watu 13 wanaoviunga mkono vikosi vya serikali na wapiganaji sita wa kundi la waasi wa Jaish al-Islam, wameuawa katika mashambulizi yaliyofanywa leo.
Mkurugenzi wa shirika hilo, Rami Abdel Rahman amesema mapigano yanafanyika katika eneo la Al-Marj ambalo ni eneo la mapambano linalodhibitiwa na waasi karibu na mji mkuu wa Syria, Damascus.
Zaidi ya raia 500 wauawa tangu kuanza mapigano
Ameongeza kusema kuwa mashambulizi ya leo ni mabaya zaidi kufanyika tangu utawala wa Syria ulipoanzisha operesheni mwezi huu wa Februari. Zaidi ya raia 500 wameuawa katika operesheni hiyo iliyoanzishwa wiki iliyopita Mashariki mwa Ghouta.
Mashambulizi hayo yanafanyika siku moja baada ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupiga kura kwa kauli moja kutaka kusitishwa mapigano nchini Syria kwa siku 30 na kuruhusu kupelekwa misaada ya kibinaadamu na kuwaondoa raia kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

0 comments:

Post a Comment