Waandamanaji hao walikuwa wakielekea ubalozi wa Marekani na makao makuu ya Tume ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS ambako waliwasilisha malalamiko yao. Kwenye malalamiko hayo, viongozi wa waandamanaji wamelaani hatua hiyo ya Marekani na kudai itadhoofisha uhuru wa nchi hiyo waliopigania na kukwamisha mchakato wa kupata ustawi.
Ijumaa iliyopita, serikali ya Marekani ilitangaza kuiwekea Sudan Kusini vikwazo, na kulihimiza Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kutekeleza zuio la kusafirisha silaha dhidi ya Sudan Kusini.
0 comments:
Post a Comment