Wednesday 28 February 2018

Syria yasitisha mapigano



Mwito wa kusitishwa mapigano kwa masaa matano uliotolewa na Urusi, katika eneo linalokaliwa na waasi nchini Syria la Ghouta Mashariki, karibu na Damascus, ili kuruhusu raia kuondoka kwenye eneo hilo umeanza kutekelezwa.
Mwito wa kusitishwa  mapigano kwa masaa matano uliotolewa na Urusi hapo jana, katika eneo linalodhibitwa na waasi nchini Syria la Ghouta Mashariki, karibu na Damascus, ili kuruhusu raia kuondoka kwenye eneo hilo, linalolengwa na mashambulizi yanayofanywa na serikali inayoungwa mkono na Urusi, umeanza kutekelezwa. Hata hivyo imeelezwa kuwa hakukua na dalili zozote za haraka za kuandaliwa kwa njia itakayotumiwa na raia hao kupita, wakati wakiondoka kwenye eneo hilo.
Rais wa Urusi, Vladimir Putin aliagiza usitishwaji mapigano wa kila siku kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana, na kuandaliwa kwa njia itakayotumika kwa ajili ya raia kupita, katika eneo hilo ambalo mashambulizi yanayofanywa na serikali yamesababisha vifo vya mamia ya raia tangu Februari 18.
Shirika linaloangazia haki za binaadamu la nchini humo limesema kumekuwepo na hali ya utulivu mashariki mwa Ghouta tangu usiku wa jana, ingawa kulirushwa maroketi manne kwenye mji wa Douma majira ya asubuhi. Kulingana na shirika hilo, watu 550 wameuawa kufuatia mashambulizi yaliyofanywa na serikali ya Syria kwa kushirikiana na Urusi.
Wizara ya ulinzi ya Urusi ilisema hapo jana kwamba kufikiwa hatua hiyo, kulifuatia makubaliano na vikosi vya Syria, kwa lengo la kuwasaidia raia kuondoka na kuwahamisha wagonjwa na majeruhi.

0 comments:

Post a Comment