Rais Donald
Trump na washirika wake katika chama cha Republican wametoa
nyaraka zenye utata za kumbukumbu wakilishutumu shirika la upepezi wa
jinai FBI kwa upendeleo na matumizi mabaya ya madaraka.
Hali hiyo inazidisha mapambano kati ya Ikulu ya White House na
waendesha mashitaka wanaochunguza kundi la kampeni ya rais.Trump alikaidi mkurugenzi wake wa FBI na wizara ya sheria na kuamuru kutolewa hadharani waraka wenye kurasa nne wa Republican , ambao unaonesha matumizi mabaya ya madaraka na kuelemea chama kimoja katika shirika hilo kubwa nchini Marekani linalolinda haki.
Mkurugenzi wa FBI Robert Mueller
"Nafikiri
ni fedheha. Kile kinachoendelea katika nchi hii, nafikiri ni
fedheha," Trump aliyeonekana kuwa katika hali ya kutofurahishwa,
alisema wakati akitangaza uamuzi wake wa kuruhusu nyaraka hizo za
kumbukumbu kutolewa hadharani. "Watu wengi wanapaswa kuona aibu na
zaidi ya hapo."Wademocrats na baadhi ya Warepublican wamelalamika kuwapo na mchezo mchafu kuhusiana na waraka huo, wakipuuzia kutolewa kwake kuwa ni kama sarakasi tu, na juhudi nyingine dhaifu kuvuruga uchunguzi kuhusiana na mahusiano kati ya timu ya kampeni ya Trump na Urusi.
Wanadai waraka huo , ulioandikwa na Devin Nunes, afisa wa mpito wa Trump, mbunge na mwenyekiti wa kamati ya bunge ya ujasusi, ina matundu makubwa. FBI binafsi imesema ina "wasi wasi mkubwa" na usahihi wa waraka huo.
Kutupiana lawama
Waraka huo unadai kwamba utafiti uliogharamiwa na chama cha Democratic ulisababisha FBI kufanya upelelezi dhidi ya msaidizi wa zamani wa Trump, Carter Page.
Katika taarifa , afisa wa habari wa Ikulu ya Marekani Sarah Sanders alisema waraka huo, "unatoa maelezo yenye wasi wasi mkubwa juu ya kuaminika kwa maamuzi yaliyofanywa katika ngazi ya juu ya wizara ya sheria na FBI.
0 comments:
Post a Comment