Saturday 3 February 2018

Trump aruhusu kutolewa kwa nyaraka za siri za FBI

Rais Donald Trump na washirika wake katika chama cha Republican wametoa nyaraka zenye utata za kumbukumbu wakilishutumu shirika la upepezi wa  jinai FBI kwa upendeleo na matumizi  mabaya ya madaraka.
Hali hiyo inazidisha  mapambano   kati ya  Ikulu  ya  White House na  waendesha  mashitaka  wanaochunguza kundi  la kampeni  ya rais.
Trump  alikaidi mkurugenzi  wake  wa  FBI  na  wizara  ya  sheria  na  kuamuru kutolewa  hadharani  waraka wenye  kurasa  nne  wa  Republican , ambao unaonesha  matumizi  mabaya  ya  madaraka  na  kuelemea  chama  kimoja katika  shirika  hilo  kubwa  nchini  Marekani  linalolinda  haki.
Robert Mueller (picture-alliance/AP/C. Dharapak)
Mkurugenzi wa FBI Robert Mueller
"Nafikiri ni fedheha. Kile  kinachoendelea  katika  nchi  hii, nafikiri  ni fedheha," Trump  aliyeonekana  kuwa katika  hali  ya kutofurahishwa, alisema wakati  akitangaza  uamuzi  wake  wa  kuruhusu nyaraka  hizo za kumbukumbu  kutolewa  hadharani. "Watu  wengi wanapaswa  kuona  aibu na  zaidi  ya  hapo."
Wademocrats  na  baadhi  ya  Warepublican  wamelalamika  kuwapo  na mchezo  mchafu kuhusiana  na  waraka  huo, wakipuuzia  kutolewa  kwake kuwa  ni  kama sarakasi  tu, na  juhudi  nyingine  dhaifu  kuvuruga uchunguzi kuhusiana  na  mahusiano  kati  ya  timu  ya  kampeni  ya  Trump  na  Urusi.
Wanadai  waraka  huo , ulioandikwa  na  Devin Nunes, afisa  wa  mpito  wa Trump, mbunge  na  mwenyekiti  wa  kamati  ya  bunge  ya  ujasusi, ina matundu  makubwa. FBI  binafsi imesema  ina "wasi wasi  mkubwa" na usahihi  wa  waraka  huo.
Devin Nunes (picture alliance/AP Photo/P.M.Monsivais) Muandishi wa waraka huo muhimu Devin Nunes
Kutupiana  lawama
Waraka  huo unadai kwamba  utafiti  uliogharamiwa  na  chama  cha Democratic  ulisababisha  FBI kufanya upelelezi dhidi  ya  msaidizi  wa zamani  wa  Trump, Carter Page.
Katika  taarifa , afisa  wa  habari  wa  Ikulu  ya  Marekani  Sarah Sanders alisema  waraka  huo, "unatoa maelezo   yenye  wasi  wasi  mkubwa  juu  ya kuaminika  kwa maamuzi  yaliyofanywa   katika  ngazi  ya  juu  ya  wizara ya sheria  na  FBI.

0 comments:

Post a Comment