Monday 19 March 2018

Rais mstaafu Mkapa ataka mjadala wa haraka kuitishwa kwa mustakabali wa elimu



 Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa akiwa jijini Dodoma amesema ni muhimu kuitishwa mjadala wa kitaifa ili kujadili hali ya elimu nchini

Amefafanua kuwa ni lazima taifa litafakari kwanini shule za serikali zinaendelea kufanya vibaya katika matokeo ya mitihani ya kitaifa kila mwaka


Aidha, Mkapa ameshauri mjadala huo uhusishe makundi yote ya jamii wakiwemo wadau kutoka sekta binafsi, wasomi pamoja na wananchi wa kawaida ili kutafuta suluhu ya kudumu ya tatizo hilo


Mkapa ambaye ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), ameyasema hayo wakati wa tukio la kumkaribisha Makamu Mkuu mpya wa Chuo Kikuu hicho, Profesa Egid Mubofu na kumuaga aliyekuwa Makamu Mkuu wa chuo aliyemaliza muda wake, Profesa Idrisa Kikula.

0 comments:

Post a Comment