Monday 19 March 2018

Teknolojia itakayotumika kombe la dunia 2018 Urusi



Shirikisho la soka duniani (FIFA) limetangaza rasmi juu ya teknolojia mpya ya kuwasaidia waamuzi kuwa itatumika katika fainali za kombe la dunia 2018 nchini Urusi. Teknolojia ya VAR inayotumika kuwasaidia waamuzi kuangalia replay na kufanya maamuzi yaliyokuwa sahihi, tayari ilikuwa imeshakubalika kutumika Afrika katika mchezo wa CAF Super Cup.
Rais wa FIFA, Gianni Infantino amethibitisha taarifa hizo wakati wa kikao cha FIFA kilichofanyika Bogota Colombia.

0 comments:

Post a Comment