Wagonjwa wa akili 55 waliokuwa wametenda makosa mbalimbali yakiwamo ya jinai, wameachiwa huru baada ya Mahakama kutowatia hatiani
Profesa Kabudi alisema kifungu cha 219(5) cha Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai, sura ya 20 kinampatia waziri wa sheria mamlaka ya kuwaachia huru wagonjwa wa akili waliotenda makosa ya jinai yakiwamo ya mauaji
Alisema kwa muda mrefu wagonjwa hao walikuwa wakihifadhiwa kwenye taasisi ya Isanga mkoani Dodoma kusubiri amri ya waziri
Aliongeza kuwa “Kutokana na hali ya afya zao za akili kuimarika, niliamua waachiwe huru ili waungane na familia zao kuendelea na matibabu wakiwa nje ya taasisi hiyo.”
0 comments:
Post a Comment