Mabingwa watetezi Yanga SC
wameendeleza wimbi la ushindi katika ligi kuu ya nchini baada ya kuibamiza Stand United goli 3-1 mchezo uliochezwa uwanja
wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga sasa imefikisha pointi 46 kwa
michezo 21. Nayo Azam FC na Tanzania Prisons FC zilmechupa katika
msimamo wa ligi hiyo baada ya kushinda mechi za ligi zilizochezwa
wikiendi iliyopita.
Klabu ya Azam imechupa hadi nafasi ya tatu wakiwa na alama 44 baada
ya kuifunga Mbao FC mabao 2-1. Nayo Prisons FC kutoka mjini Mbeya,
wamepanda hadi nafasi ya nne baada ya ushindi wa goli 2-1 dhidi ya
Mtibwa Sugar kutoka Morogoro kwenye Uwanja wa Sokoine.
0 comments:
Post a Comment