Paka mmoja maarufu
ambaye anadaiwa kuwa na uwezo wa kipekee wa kutabiri ametabiri mshindi
wa mechi ya kwanza ya Kombe la Dunia nchini Urusi.
Achilles, paka wa rangi nyeupe ambaye ni kiziwi, hubashiri mshindi kwa kuchagua katika ya bakuli mbili ambazo zimewekwa bendera za mataifa yanayocheza.
Paka huyo ni miongoni mwa paka wanaofugwa kukabiliana na panya katika makumbusho ya Hermitage mjini St Petersburg, ingawa sasa ana majukumu hayo mapya.
Anadaiwa kubashiri kwa ufasaha mshindi wa Kombe la Mashirikisho mwaka 2017.
Paka huyo alitoa utabiri wake wa sasa Jumatano.
Baada ya mashindano ya Kombe la Dunia mwaka huo pweza Paul alitokea kwenye video akiipigia debe Uingereza kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia 2018.
Paul alifariki Oktoba mwaka 2010 kifo cha kawaida kulingana na hifadhi ya Oberhausen nchini Ujerumani.
0 comments:
Post a Comment