Mwanamke mmoja amelazwa katika hospitali ya Leratong baada ya kukutwa hai katika jokofu kwenye chumba cha kuhifadhia maiti
Mfanyakazi katika chumba hicho aligundua bado mwanamke huyo anapumua wakati alipofika kuutizama mwili na kutayarisha nyaraka kumhusu
Mwanamke huyo alifikishwa katika chumba hicho baada ya madaktari kusema amefariki kutokana na kutoonesha dalili zozote za uhai kufuatia ajali ya barabarani aliyoipata
Familia ya mwanamke huyo imesema wamepata mshtuko mkubwa na wana wasiwasi kuhusu mkasa huo hivyo wanahitaji ufafanuzi ni vipi makosa hayo yanaweza kutokea
0 comments:
Post a Comment