Thursday 12 July 2018

Manchester City yamsajili Riyad Mahrez


Mabingwa wa ligi kuu England msimu wa 2017/2018 club ya Man City usiku wa July 10 2018 wametangaza rasmi kunasa saini ya staa mpya katika club yao, Man City ambao wanajiandaa na msimu wa 2018/19 ili kutetea taji lao wanazidi kuboresha kikosi chao kwa kufanya usajili.
Man City wamefanikiwa kumsajili winga wa kimataifa wa Algeria anayeichezea club ya Leicester City ya England Riyad Mahrez kwa mkataba wa miaka mitano,
Riyad Mahrez ameondoka Leicester na kujiunga na Man City kwa kiasi cha dau linalotajwa kufikia pound milioni 60.

0 comments:

Post a Comment