Thursday 16 November 2017

Hali yakuwa ya kuogopesha Zimbabwe


Rais Robert Mugabe amesisitiza kwamba atasalia kuwa mtawala pekee halali wa taifa hilo, kimesema chanzo kimoja cha kijasusi, huku akimkataa Padri Fidelis Mukonori kusimamia mazungumzo ya upatanishi.
BG Mugabe wurde Premierminister 18.04.1980 (picture-alliance/abaca/G. Buthaud)
Rais Robert Mugabe amesisitiza kwamba atasalia kuwa mtawala pekee halali wa taifa hilo, kimesema chanzo kimoja cha kijasusi leo hii, huku akimkataa padri wa kanisa Katoliki Fidelis Mukonori kusimamia mazungumzo ya upatanishi yatakayoruhusu mpiganaji huyo wa zamani wa msituni mwenye umri wa miaka 93, kuondoka kwa amani baada ya mapinduzi ya kijeshi. 
Padri huyo, Fidelis Mukonori, atakuwa kama kiunganishi kati ya Rais Mugabe na majenerali wa jeshi, ambao walikamata mamlaka jana Jumatano, katika kile kinachoelezwa kama operesheni dhidi ya "wahalifu" miongoni mwa watu walio ndani ya utawala wake, mwanasiasa mwandamizi ameliambia shirika la habari la Reuters.  
Chanzo hicho hakikufafanua zaidi kuhusu mazungumzo hayo, ambayo yanaonekana yana lengo la kufanikisha hatua ya kukabidhi madaraka kuwa ya amani na kutogubikwa na machafuko baada ya kuondoka kwa Mugabe, ambaye ameliongoza taifa hilo tangu uhuru wake mwaka 1980. 
Ripoti za kijasusi za Zimbabwe zilizoonwa na shirika la habari la Reuters, zinahitimisha kwamba mkuu wa zamani wa usalama wa taifa, Emmerson Mnangagwa, aliyefukuzwa akiwa makamu wa rais mwezi huu, amekuwa akifanya mipango na jeshi na upande wa upinzani kwa zaidi ya mwaka mmoja, ya namna ya kumuondoa Mugabe madarakani. 
Kurejea kwa kiongozi wa upinzani Morgan Tsvangirai nako kunaelezwa kama kunachochea minong'ono kwamba mipango hiyo inawezekana itaanza kutekelezeka. Tsvangirai amekuwa nchini Uingereza na Afrika Kusini akipata matibabu ya saratani, na amerejea mjini Harare jana Jumatano, amesema msemaji wa kiongozi huyo
Alpha Condé (Getty Images/M. Medina)
Rais wa Guinnea na mkuu wa Umoja wa Afrika, AU, Alpha Conde, ameitaka Zimbabwe kuitii katiba ya nchi
Umoja wa Afrika waitaka Zimbabwe kuzingatia katiba ya nchi.
Alipozungumza na kituo cha televisheni cha shirika la habari la Ujerumani la DW, pembezoni mwa mkutano unaohusu mabadiliko ya hali ya hewa mjini Bonn, rais wa Guinnea ambaye pia ni mkuu wa Umoja wa Afrika, Alpha Conde kuhusiana na hali ilivyo nchini humo, amesema.

0 comments:

Post a Comment