Thursday 16 November 2017

Wasifu wa Rais Mugabe

Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe
Robert Mugabe alizaliwa tarehe 21 mwezi Februari mwaka wa 1924 katika kijiji kilichokuwa karibu na mji mkuu wa sasa Harare,  wakati huo ukijulikana kama Salisbury. Alisomea taaluma ya ualimu na anaaminika kuwa na jumla ya shahada saba kutoka vyuo vikuu.
Mwanasiasa huyo alipata umaarufu mkubwa kwa mara ya kwanza pale alipoongoza vita vya msituni dhidi ya wakoloni walioitawala Zimbabwe, wakati huo ikijulikana kama Rhodesia.
Mugabe alikamatwa na kufungwa jela kwa kipindi cha miaka kumi kufuatia hotuba aliyoitoa manamo mwaka wa 1964, iliyowagadhabisha wakoloni ambao waliitaja kuwa ya uchochezi.
Aliachiliwa kutoka jela mnamo mwaka wa 1974 na kuingia kwenye siasa za kushinikiza Waingereza kusitisha utawala wake kwa Rhodesia.
Baadaye Mugabe alitorokea nchi jirani ya Msumbiji na kurudi Rhodesia mnamo mwaka wa 1979.
Baada ya Zimbabwe kupata Uhuru wake mwaka wa 1980, Mugambe alichuka nafasi ya waziri mkuu, na kwendelea kuongoza nchi hiyo chini ya chama tawala cha Zanu PF.
Katika miaka ya mwanzo wa uongozi wake, Mugabe alisifika kwa upanuzi wa miundo msingi na huduma za kijamii, zikiwepo hospitali na shule za nchi hiyo.
Hali kadhalika, alishutumiwa kwamba aliwanyanyasa wapinzani wake, wakiongozwa na kiongozi wa upinzani wa wakati huo, Joshua Nkomo.
Tume ya kanisa katoliki kuhusu haki na amani ilitoa ripoti iliyodai kwamba Zaidi ya watu 20,000 walipoteza maisha yao chini ya utawala wa Mugabe.
Mugabe alichukua wadhifa wa urais mnamo mwaka wa 1987 baada ya nafasi ya waziri mkuu kuondolewa rasmi.
Tangu wakati huo ameshinda uchaguzi mara nyingi licha ya kutajwa na wapinzani wake na waandgalizi mbali mbali kama uliojawa na udanganyifu na usiokuwa wa haki na kweli.
Mke wake wa kwanza, Sally Hayfron, mzawa wa Ghana, alifariki mnamo mwaka wa 1992 kutokana na ugonjwa wa figo.
Mugabe alimuoa mkewe wa sasa, Grace Mugabe, mnamo mwaka wa 1996.
Wakososaji wa rais huyo wametaja hatua yake ya mageuzi juu ya umiliki wa ardhi kama moja ya masuala muhimu yaliyochangia hali ya kuzorota vibaya kwa uchumi wa nchi hiyo.
Aidha, mwanasiasa huyo mkongwe amekosolewa kwa kile wapinzani wake wamekiita kukatalia madarakani, kuwanyanyanyasa wapinzani wake wa kisiasa, kumfuta kazi makamu wake na kuunga mkono azima ya mkewe ya kutaka kuwa rais wa Zimbabwe, kati ya mambo mengine yaliyozua utata

0 comments:

Post a Comment