Saturday 18 November 2017

ZANU PF yamshinikiza Mugabe ajiuzulu


Chama tawala Zimbabwe ZANU PF kimemtaka Rais Robert Mugabe ajiuzulu. Gazeti la Herald limeandika kuwa matawi ya chama hicho katika majimbo yote10 yalikutana Ijumma na yamemtaka Mugabe na mke wake Grace wajiuzulu.
Simbabwe Harare Robert Mugabe (picture-alliance/AP Photo/B. Curtis)
Viongozi wa chama hicho wamesema watamshinikiza kiongozi huyo ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 1980 kuondolewa kutoka uongozi wa chama hicho ifikapo hapo kesho Jumapili, na baada ya hilo, bunge litapiga kura ya kutokuwa na imani naye.
Chama cha ZANU PF kitafanya mkutano maalamu wa kamati kuu siku ya Jumapili kujadili yanayojiri kisiasa nchini humo.
Mugabe alionekana kwa mara ya kwanza hadharani, katika mahafali ya chuo kikuu mjini Harare siku ya Ijumaa (17.11.2017) tangu jeshi lilipomuweka chini ya kifungo cha nyumbani wiki hii. Mkewe Grace hajaonekana hadharani tangu jeshi lilipochukua madaraka.
Jeshi la Zimbabwe linapata ugumu wa kuonyesha heshima kwa kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 93 kwa kumuita rais na kamanda mkuu wa jeshi.
Madaraka mikononi mwa Jeshi
Taarifa kutoka kwa jeshi hilo imesema kuwa viongozi wake wanashauriana na Kamanda Mkuu wa jeshi Rais Robert Mugabe kuhusu njia bora ya kusonga mbele na litalifahamisha taifa baadaye kuhusu matokeo hayo haraka iwezekanavyo.

0 comments:

Post a Comment