Jeshi la Uganda limelaani
shambulizi lililofanywa na waasi wa kundi la ADF dhidi ya jeshi la
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (FARDC), na kusababisha vifo vya askari
watatu na wengine watano kujeruhiwa.
Msemaji wa jeshi la Uganda Bw. Richard Karemire amesema, kitendo hicho cha ADF hakitazuia jitihada za kikanda za kuliondoa kundi hilo. Jeshi la Uganda UPDF litaendelea kushirikiana na jeshi la serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuwafukuza wale wanaovuruga amani ya ya kikanda.
Habari zinasema, waasi wa ADF walishambulia kambi ya jeshi la serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ya Muzambay katika jimbo la Kivu Kaskazini baada kufukuzwa na jeshi la Uganda.
Msemaji wa jeshi la Uganda Bw. Richard Karemire amesema, kitendo hicho cha ADF hakitazuia jitihada za kikanda za kuliondoa kundi hilo. Jeshi la Uganda UPDF litaendelea kushirikiana na jeshi la serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuwafukuza wale wanaovuruga amani ya ya kikanda.
Habari zinasema, waasi wa ADF walishambulia kambi ya jeshi la serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ya Muzambay katika jimbo la Kivu Kaskazini baada kufukuzwa na jeshi la Uganda.
0 comments:
Post a Comment