Friday 9 February 2018

ANC yakanusha ripoti kwamba rais Zuma atajiuzulu jumamosi



Chama tawala cha Afrika Kusini ANC kimekanusha ripoti za vyombo vya habari kuwa rais Jacob Zuma atajiuzulu jumamosi na kusema taarifa hizo si sahihi na ni za kupotosha.
Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya mratibu mkuu wa chama hicho kwenye bunge imesema, chama cha ANC hakihusiki na taarifa kuwa mwenyekiti wa chama hicho Bw. Cyril Ramaphosa amekiambia kikundi cha uongozi wa bunge kuwa rais Zuma atajiuzulu jumamosi na hatapewa kinga.
Mapema jana, vyombo vya habari vya Afrika Kusini viliripoti kuwa Bw. Ramaphosa aliambia kikundi cha uongozi cha bunge kuwa kinga kwa rais Zuma sio sehemu ya mjadala huo.
Ripoti hizo zilitolewa baada ya Bw. Ramaphosa kuwataka wananchi kutulia wakati wakijadili masuala husika na rais Zuma.

0 comments:

Post a Comment