Polisi nchini
Israel imesema Waziri mkuu wa nchi hiyo Benjamin Netanyahu anapaswa
kushtakiwa na mashtaka ya rushwa yanayomkabili.
Taarifa
iliyotolewa na polisi imesema, wana ushahidi wa kutosha kumtia hatiani
Bwana Netanyahu kwa rushwa, ufisadi na kuvunjwa uaminifu katika kesi
mbili tofauti.Waziri mkuu wa Israel anatuhumiwa kwa kutaka gazeti la nchi hiyo la Yediot Aharonot kuchapisha taarifa yake kwa upendeleo, ikiwa kama takrima kulisaidia kuweza kudhibiti magazeti yanayoshindana nayo.
Polisi wanasema mhariri wa gazeti hilo Arnon Mozes naye pia anapaswa kushtakiwa.
Madai mengine ni kwamba Waziri huyo mkuu aliyeongoza nchi hiyon toka mwaka 2009 alipokea zawadi ya kiasi cha dola 283,000 kutoka kwa msanii wa Hollwood Mogul Arnon Milchan na washabiki wengine, ili kuweza kumsaidia kupata Visa ya marekani.
0 comments:
Post a Comment