Shirika hilo limesema, upitishwaji wa haraka wa muswada wa sheria wa kuanzisha Eneo hilo kunaonyesha nia thabiti ya kisiasa ya serikali ya Kenya katika kuimarisha mwingiliano wa Afrika kuhusu biashara kupitia kuondoa vikwazo vya kibiashara ili kukuza soko moja huru katika bara hilo.
Nchi zote za Afrika Mashariki, isipokuwa Burundi ambayo haikuhudhuria mkutano wa kilele Umoja wa Afrika uliofanyika mwezi uliopita nchini Rwanda, zimesaini itifaki zote tatu zilizopitishwa katika mkutano huo.
0 comments:
Post a Comment