Friday 6 April 2018

Sierra Leon Yapata rais mpya



Rais mteule kutoka chama kubwa zaidi cha upinzani cha Sierra Leone cha SLPP, Bw. Julius Maada Bio ameapisha kuwa rais mpya jana usiku mjini Freetown mara baada ya kushinda kwenye uchaguzi mkuu.
Tume ya uchaguzi ya Sierra Leone jana imetangaza matokeo ya duru ya pili ya upigaji kura ambapo Bw. Bio amepata asilimia 51.8 ya kura na kumshinda mgombea kutoka chama tawala Bw. Samura Kamara aliyepata asilimia 48.19 ya kura.
Habari zinasema, watu zaidi ya milioni 2.5 wa Sierra Leone wameshiriki kwenye upigaji kura huo ambapo kiwango cha upigaji kura kimefikia asilimia 81.11.

0 comments:

Post a Comment