Friday 4 May 2018

Wanahabari zaidi ya 44 wadaiwa kuuwawa duniani


Jana ikiwa ni siku ya habari duniani, Shirika la kutetea haki za wanahabari Press Emblem Campaign PEC limesema idadi ya wanahabari waliouawa katika miezi minne ya mwanzo mwaka huu imefikia 44 katika nchi 18, ikiwa ni ongezeko la asilimia 57 kuliko mwaka jana kipindi kama hicho.

Kwenye taarifa yake, PEC inalaani kuongezeka kwa wanahabari wahanga wakati dunia inaadhimisha Siku ya uhuru wa vyombo vya habari.
Kwa mujibu wa PEC, nchi zenye hatari kubwa zaidi kwa wanahabari tangu mwanzoni mwa mwaka huu ni Afghanistan, Mexico, Syria, Ecuador, India na Yemen

0 comments:

Post a Comment