Sunday 3 December 2017

Mohammed Dewji ashinda zabuni ya uwekezaji Simba SC ,aahidi mabadiliko


Mfanyabiashara maarufu nchini Tanzania, Mohammed Dewji ameshinda zabuni katika mchakato wa kumtafuta muwekezaji wa klabu ya Simba na ofa yake ya Tsh bilioni 20.

Dewji ambaye amejitokeza na kuwa muwekezaji pekee ambaye aliweka dau kubwa la Tsh bilioni 20 kupata hisa kwa asilimia 51 ndani ya klabu hiyo amekubaliwa kwa dau hilo kwa kupata hisa 49.

Mwenyekiti wa kamati ya mchakato huo wa mabadiliko, Jaji Mihayo amesema, Mo Dewji amepita na kitachofuatia ni majadiliano mengine baada ya mkutano wa leo.

“Mohammed Dewji ndiye mshindi, maana katika kamati yetu. Hivyo yeye ndiye amekuwa mshindi wa kuwania kuwekeza katika klabu ya Simba. Baada ya mkutano huu kutakuwa na majadiliano,” amesema Jaji Mihayo. 
 
Katika hotuba yake iliyoshiba mabadiliko ndani yake mfanyabiaashara huyo amehaidi kufanya makubwa ambayo uongozi wa simba haujawahi kufanya vitu alivyohaidi ni kama viwanja vya kisasa ,hostel bora pamoja na kuwa na Tv simba itakayotumika katika kuitangaza timu hiyo.

0 comments:

Post a Comment