Mvua kubwa ilianza kunyesha katika baadhi ya maeneo ya Mindanao ijumaa na kusababisha mafuriko ya ghafla na maporomoko ya udongo katika eneo hilo. Watu elfu 98, wengi wakitoka familia za wakulima zenye hali duni ya kiuchumi, walisherehekea sikukuu ya Krismas katika vituo vya uokoaji vilivyowekwa na serikali.
Tume ya Kudhibiti Majanga nchini humo imesema, baadhi ya wakazi walipuuza wito wa serikali wa kuondoka kwenye maeneo yao kabla ya mvua hiyo kunyesha. Tume hiyo imesema barabara, madaraja, na mashamba yameharibiwa vibaya na mvua hiyo.
0 comments:
Post a Comment