Tuesday 12 December 2017

Tuzo za Nobel za mwaka 2017 zafanyika huko Stockholm



Sherehe ya kutoa tuzo za Nobel za mwaka 2017 katika sekta za fizikia, kemikali, saikolojia au matibabu, fasihi na uchumi imefanyika jana huko Stockholm nchini Uswiss na kuhudhuriwa na watu zaidi 1,500 wakiwemo wajumbe wa familia ya kifalme, viongozi na wajumbe wa sekta mbalimbali.
Katika salamu zake za pongezi, Mwenyekiti wa Shirika la Mfuko la Nobel Bw. Carl-Henrik Heldin amesema, dunia inakabiliana na changamoto nyingi, na baadhi ya watu wana mashaka juu ya fikra ya sayansi na mantiki na utafiti wa elimu mpya. Amesema maadili ya binadamu, umakinifu na utafiti wa elimu mpya yanayoheshimiwa na Nobel yanapaswa kuwa msingi wa uamuzi na vitendo vya binadamu katika maisha binafsi na shughuli za siasa na biashara.

0 comments:

Post a Comment