Monday 22 January 2018

Chama cha upinzani Ujerumani SPD chaunga mkono mazungumzo na Merkel


Chama cha  Social Democratic SPD kimepiga  kura kuunga  mkono  kuanza  kwa mazungumzo  ya  mwanzo  ya  kuunda  serikali  ya  mseto na  chama  cha kansela Angela Merkel.
Außerordentlicher SPD-Parteitag Abstimmung über Große Koalition (picture alliance/dpa/K. Nietfeld
) Wajumbe wa SPD wakipiga kura kuunga mkono mazungumzo na chama cha Merkel
Hatua  hiyo  imeliingiza  taifa  hilo  ambalo  ni  uchumi  mkubwa  katika  bara  la Ulaya  hatua  moja  karibu  na   kupata  serikali  imara  baada  ya miezi  kadhaa ya  hali  ya sintofahamu  ya  kisiasa.
Wajumbe  wa  chama  cha  SPD walipiga  kura  362 za  'ndio'  dhidi  ya  kura  279  za 'hapana" kusongambele  na  majadiliano  baada  ya  viongozi  wa  chama  hicho  cha  siasa za  wastani  zan  mrengo  wa  kushoto  kukubali  muongozo wa  muungano  pamoja  na  kundi la  vyama  vya  kihafidhina  vinavyoongowa  na  kansela  Merkel  mapema  mwezi  huu. Hakuna  mjumbe  aliyejizuwia  kupiga  kura.
Außerordentlicher SPD-Parteitag SPD-Parteivorsitzender Martin Schulz (picture alliance / Federico Gambarini/dpa) Kiongozi wa chama cha SPD Martin Schulz
Mazungumzo  yanatarajiwa  kuanza  wiki  hii, na  kuleta ahueni  kwa  washirika  wa  Ujerumani barani  Ulaya , ambako  Merkel  kwa  muda  mrefu  amechukua  nafasi  ya  uongozi  katika masuala  ya  kiuchumi  na  usalama. Wajumbe  wa  chama  cha  SPD  bado  watakuwa  na nafasi  ya  kupiga  kura  katika  makubaliano  ya  mwisho  ya  kuunda  serikali , kama yatapatikana.
Kiongozi  wa  chama  cha  Social Democratic SPD Martin Schultz  hapo  awali  katika hotuba  yake  kwa  wajumbe aliwataka wanachama wa chama  hicho kupiga kura kwa  ajili ya  kufungua  mazungumzo  ya  kuunda  serikali ya  mseto na  chama  cha  kansela  Merkel, akisema  serikali  imara  ya  Ujerumani  inahitajika  kuimarisha  Ulaya  na  kuwa kama  ukuta dhidi  ya  siasa  kali za  mrengo wa  kulia.
Außerordentlicher SPD-Parteitag
a Abstimmung (Reuters/W. Rattay) Mkutano wa chama cha SPD mjini Bonn
Uamuzi wake ulikuwa sahihi
Chama  hicho  cha  siasa za wastani  za  mrengo  wa  kushoto  kimeshiriki  katika  serikali na  kundi  la  vyama  vya  kihafidhina  la  kansela  Angela  Merkel  tangu  mwaka  2013, lakini Schultz aliapa  kutorejea  tena  katika  kile  kinachoitwa "muungano  mkuu" baada  ya  chama chake  cha  Social Democratic kupata  kipigo  katika  uchaguzi  wa  mwezi  Septemba.

0 comments:

Post a Comment