Ziara ya kutembeza tuzo halisi ya
ubingwa wa kombe la dunia kwenye mchezo wa soka imeanza rasmi jana mjini
London nchini Uingereza na tuzo hiyo ikitarajiwa kupitishwa katika miji
91 ya mataifa 51 katika mara yote Duniani.
Hapa Beijing kombe hilo litapita Aprili 25 kabla ya kwenda Shanghai
Aprili 26, kwa nchi za Afrika Mashariki kombe hilo litatua Nairobi
nchini Kenya Februari 26, na Kampala Uganda mwezi Machi 5.
Lengo la ziara ya kombe hilo, kwa mujibu wa waratibu ni kuwapelekea kwa ukaribu zaidi wapenzi na mashabiki wa soka kombe halisi, lakini pia ikiwa ni kuitangaza michuano ya kombe la dunia ijayo itakayofanyika nchini Urusi mwezi Juni mwaka huu.
Lengo la ziara ya kombe hilo, kwa mujibu wa waratibu ni kuwapelekea kwa ukaribu zaidi wapenzi na mashabiki wa soka kombe halisi, lakini pia ikiwa ni kuitangaza michuano ya kombe la dunia ijayo itakayofanyika nchini Urusi mwezi Juni mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment