Monday 12 February 2018

Liverpool yajikongoja kuifikia Manchester United


Magoli mawili yaliyofungwa na wachezaji Mohamed Salah, pamoja na Roberto Firmino jana kwenye mechi dhidi ya Southampton, yameifanya Klabu ya Liverpool ipunguze tafauti ya pointi kati yake na Manchester United kwenye msimamo wa ligi kuu nchini Uingereza.
Kwa ushindi huo, Liverpool sasa imefikisha jumla ya pointi 54 na inakamata nafasi ya tatu nyuma ya Manchester United yenye 56.
United imekwama katika pointi 56 baada ya jana kukubali kipigo cha goli 1-0 ilipocheza dhidi ya Newcastle United, ambapo goli hilo lilifungwa na Matt Ritchie katika dakika ya 65 kwenye uwanja wa St. James Park.
Matokeo mengine katika mechi za ligi hiyo zilizopigwa jana, Huddersfield ilipata ushindi wa magoli 4-1 ilipocheza dhidi ya AFC Bournemouth

0 comments:

Post a Comment