Michezo
ya marudiano ya robo fainali ya UEFA Champions League msimu wa
2017/2018 imeendelea tena usiku wa kuamkia leo kwa michezo miwili
kuchezwa, AS Roma wakiwa nyumbani wameushangaza ulimwengu baada ya
kuitoa FC Barcelona, mchezo wa kwanza wa Roma dhidi ya Barcelona
uliyochezwa Nou Camp ulimalizika kwa Barcelona kupata ushindi magoli
4-1, hivyo Roma kupata ushindi wa magoli 3-0 kumewafanya wafuzu hatua ya
nusu fainali kwa ushindi wa jumla ya magoli 4-4 ila goli la ugenini
ndio linawabeba.
Liverpool wakaibuka kidedea cha mabao 2-1 dhidi ya Man City na sasa
Jurgen Klopp anakuwa kocha wa kwanza kuwahi kumfunga Pep Gurdiola
michezo 3 katika msimu mmoja wa ligi na hiki kikiwa kipigo cha 3 kwa
City mfululizo.
0 comments:
Post a Comment