Monday 7 May 2018

Watu 10 wafariki dunia katika shambulio la Afghanistan



Takribani watu 10 wamefariki dunia na wengine 29 kujeruhiwa baada ya kutokea kwa mlipuko wa bomu katika Msikiti mmoja Mashariki mwa nchi hiyo

Mlipuko huo umetokea wakati Watu wakiwa wamekusanyika kwaajili ya sala ya -
Msikiti huo pia hutumika kama Kituo cha Kujiandikisha Kupiga Kura ya Wabunge katika Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu

Tukio hili(mlipuko) ni la pili katika kipindi cha muda mfupi. Ikumbukwe kuwa Jumapili iliyopita katika Mji wa Kabul ilitokea milipuko miwili iliyosababisha vifo vya Watu zaidi ya 100

Mpaka sasa hakuna kikundi chochote kilichotoa taarifa ya kukiri kuhusika na shambulio hilo

0 comments:

Post a Comment