Thursday 23 November 2017

Mjue Pablo Picasso mchoraji maarufu Duniani


Pablo Picasso
Signatur Pablo Picasso
Pablo Ruiz Picasso (25 Oktoba 1881 - 8 Aprili 1973) alikuwa mchoraji mashuhuri na pia mchongaji wa Hispania. Jina lake kamili ni Pablo Diego José Francisco de Paula Juan Nepomuceno María de los Remedios Cipriano de la Santísima Trinidad Clito Ruiz y Picasso.

Umuhimu wa Picasso

Picasso anahesabiwa kati ya wasanii wakuu wa karne ya 20. Alibadilisha uzoefu jinsi ya kuona dunia katika utamaduni wa Kimagaharibi wa Ulaya na Marekani. Mtindo wake wa uchoraji ulianza kutumia maumbo ya jiometria. Katika hatua hii aliathiwirwa na sanaa ya Afrika.
Kipindi cha buluu: Picha ya Suzanne Bloch (1904)
Picasso hakuwa mchoraji wa kwanza wala mchoraji wa pekee aliyetumia mibinu mipya lakini alijulikana kushinda wote na ile "sanaa ya kisasa" ilitambulishwa mara nyingi kwa lugha ya "picha kama Picasso".

Mwanzo wa kazi

Picasso alianza kuchora kwa umri mdogo wa miaka saba akisaidiwa na babake aliyekuwa mwalimu wa sanaa. Akiwa na miaka 10 aliandikishwa kwenye chuo cha sanaa na 1895 alipokelewa kwenye chuo kikuu cha sanaa huko Barcelona.
Alitembelea sana makumbusho penye taswira na sanamu za wasanii waliotangulia. Alipenda kusafiri penye maonyesho makubwa kama Madrid au Paris.
Taswira zake za awali badi zililingana zaidi na picha jinsi zilivyokuwa kawaida. Mwanzoni alipenda rangi ya buluu na mfano wake ni picha ya Suzanne Bloch hapo chini.
Baada ya kuona sanaa ya Afrika: Mabinti wa Avignon (1910)

Athira ya Kiafrika na mtindo mpya

Mjini Paris alikuta maonyesho ya sanaa ya Kiafrika iliyomwathiri sana. Hii inaonekana katika "Mabinti wa Avignon" (1910).
Baadaye aliendelea kuvunja maumbile ya kawaida na kuyajenga upya kwa kutumia maumbo ya kijiometria. Mtindo huu uliitwa "cubisme" kwa Kifaransa yaani "umchemraba" kutokana na mchemraba kama umbo la kijiometria linalotumiwa kujenga upya maumbile ya yale yanayoonyeshwa kwenye picha.
Ukubisti (uchembemraba): Picha ya Juan Gris (1912)
Picasso aliendelea kujaribu mitindo mpya-mpya. Kati ya taswira zake zilikuwa maarufu sana kimataifa ilikuwa "Guernica" (1937) iliyonesha kikuli na maafya ya vita. Ilichorwa wakati wa vita ya wenyewe kwa wenyewe ya Hispania baada ya shambulio la wanahewa Wajerumani dhidi ya mji mdogo wa Guernica.
Kwa jumla imekadiriwa ya kwamba Picasso aliumba kazi za sanaa zaidi ya 20,000 kama vile taswira, picha za mchapo na sanamu.

Maisha ya binafsi

Picasso alioa mara mbili lakini alikuwa na wapenzi wengi. Alizaa watoto wanne na wake watatu.
"Guernica" (1937) imechorwa baada ya kuangamizwa kwa mji wa Guernica
Baada ya kuhamia Paris alibaki huko akakataa kurudi Hispania kwa sababu alimchukia dikteta Francisco Franco. Wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia alikaa Paris chini ya utawala wa Wajerumani na wakati ule hakuweza kuonyesha kazi zake kwa sababu siasa ya Ujerumani ilichukia mtindo wake. 1945 alijiunga na chama cha Kikomunisti abakabi mkomunisti hata kama pia siasa ya Umoja wa Kisovyeti haikupenda mtindo wake.
Tangu 1961 aliishi katika Ufaransa ya Kusini alipoaga dunia 1973. Aliacha taswira maelfu ya akiacha

0 comments:

Post a Comment