Monday 23 April 2018

Idadi ya vifo yaongezeka baada ya shambulizi Afghanistan


Wizara ya afya ya umma ya Afghanistan imesema mlipuko uliotokea jana karibu na kituo cha kuandikisha wapiga kura mjini Kabul, umesababisha vifo vya watu 57 na wengine 119 kujeruhiwa. Kwa mujibu wa wizara hiyo, wengi wa waliouawa ni raia wa kawaida, wakiwemo wanawake 21 na watoto watano, na kundi la Islamic State limetangaza kuwajibika na shambulizi hilo. Imefahamika kuwa uchaguzi wa bunge nchini Afghanistan utafanyika Oktoba 20 mwaka huu, na kazi ya kuandikisha wapiga kura imeanza Aprili 14 kote nchini humo.

0 comments:

Post a Comment