Friday 13 April 2018

Umoja wa Mataifa walaani matumizi ya silaha za kemikali Syria



Umoja wa Mataifa(UN) umezionya nchi zenye nguvu kutoruhusu mzozo kuhusu madai ya matumizi ya silaha za sumu dhidi ya Syria kuongezeka

Kutokana na hali ya wasiwasi kuhusu mvutano huo wa Syria, mkutano wa faragha wa dharura wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa utafanyika baadae leo

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amesema hadi sasa Baraza la Usalama la umoja huo limeshindwa kufikia makubaliano ya kidiplomasia kuhusu Syria

Urusi na Marekani hadi sasa zimepiga kura ya turufu kupinga azimio la kila mmoja la kutaka kuanzisha uchunguzi wa kimataifa kuhusu matumizi ya silaha za sumu

Shirika la kimataifa la kudhibiti silaha za sumu, OPCW, limesema hivi karibuni litapeleka timu yake ya wachunguzi kwenye mji wa Douma kwa ajili ya kufanya uchunguzi

0 comments:

Post a Comment