Sudan imesema jeshi lake liko tayari kukabiliana na tishio lolote la usalama linaloweza kutokea kwenye eneo la mpaka wa mashariki mwa nchi hiyo.
Akikutana na mwenzake wa Ethiopia Bw. Workneh Gebeyehu, waziri wa
mambo ya nje wa Sudan Bw. Ibrahim Ghandour amesema, wamegundua kuwa
kuna nchi inajaribu kuwadhuru, na jeshi la Sudan limepanga upya vikosi
vyake ili kukabiliana na kitendo chochote kitakachoharibu usalama wa
Sudan.
Kwa upande wake Bw. Gebeyehu amesema, Ethiopia inapenda kukuza uhusiano wa pande mbili kati yake na Sudan, na kuendelea kusaidia kuhimiza amani katika kanda hiyo.
Kwa upande wake Bw. Gebeyehu amesema, Ethiopia inapenda kukuza uhusiano wa pande mbili kati yake na Sudan, na kuendelea kusaidia kuhimiza amani katika kanda hiyo.
0 comments:
Post a Comment