Sunday, 24 December 2017

Jenerali aliyemfanya Mugabe Kujiuzulu apewa wadhifa Zanu-PF

 

Jenerali wa Zimbabwe, aliyeongoza mapinduzi yaliyopelekea Robert Mugabe kuondoshwa madarakani, ameteuliwa kuwa naibu kiongozi wa chama tawala cha ZANU-PF.
Uteuzi huo ulifanywa na rais mpya wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa.
Constantino Chiwenga, alistaafu hivi karibuni kama mkuu wa jeshi, na kuzusha tetesi, kwamba atapewa wadhifa wa kisiasa.
Uteuzi huo, unaonekana kama hatua ya kuelekea kutajwa kuwa makamo rais.Makamu mwengine wa Zanu PF ni Kembo Mohadi ambaye alikuwa waziri usalama chini ya Robert Mugabe.
Hatua hiyo ya uchukuaji mamlaka mnamo tarehe 15 Novemba inajiri siku kadhaa baada ya Mnangagwa ,wakati huo akiwa makamu rais alifutwa kazi na Mugabe na kuondoka nchini humo.

Hatua hiyo ilionekana kama jaribio la kumuweka mke wa Mugabe kuwa mrithi wake badala ya Mnangagwa.
Lakini bwana Mnangagwa alikuwa na uhusiano mkubwa na Jeshi na kufuatia kuingilia kati kwa jeshi aliteuliwa kuwa rais na kuapishwa tarehe 24 mwezi Novemba.

0 comments:

Post a Comment

Throne