Rais Mnangagwa amesema anatarajia kampenzi zitafanyika kwa ushindani, amani na kuwawezesha Wazimbabwe kuchagua kwa uwazi na kidemokrasia. Amesema anatarajia upande wa upinzani utafanya kampeni kwa utulivu bila ghasia, na kuwaruhusu watu wa Zimbabwe kuamua mwelekeo ambao Zimbabwe itaufuata katika miaka mitano ijayo.
Wakati huohuo, aliyekuwa waziri katika serikali ya rais wa zamani wa nchi hiyo Robert Mugabe, Bw. Ambrose Muyinhiri amejiuzulu wadhifa wake wa ubunge akipinga kuondolewa madarakani kwa rais huyo mwezi Novemba mwaka jana.
0 comments:
Post a Comment