Nchini Israel Takribani raia wa Palestina 41 wameuawa na wengine 1,300 kujeruhiwa ambapo 450 kati yao wamepata majeraha ya risasi zilizorushwa na Wanajeshi wa Israeli
Raia wa Palestina takribani 35,000 waliandamana Ukanda wa Gaza wakipinga ufunguzi wa Ubalozi wa Marekani katika mji wa Jerusalem
Makao makuu ya Israeli yalihamishwa kutoka Tel Aviv na kupelekwa Jerusalem na mnamo mwezi Desemba mwaka jana Rais wa Marekani, Donald Trump alitangaza kuutambua mji wa Jerusalem kama Makao makuu ya Israeli
Kati ya waliouawa ni mtoto wa miaka 14 huku mauaji haya yakitajwa kuwa mabaya na yakutisha zaidi tangu mwaka 2014
Wakati haya yakijiri, ujumbe maalum kutoka Ikulu ya Marekani ulioambatana na Mtoto wa rais Trump na Mumewe walikuwa wakishuhudia ufunguzi huo wa ubalozi pamoja na Waziri Mkuu wa Israeli, Benjamin Netanyahu.
0 comments:
Post a Comment